Sunday, 13 December 2015

KUMBE HIKI NDICHO KIPAJI KINGINE CHA YAYA TOURE UKITOA MPIRA WA MIGUU, KITAZAME HAPA.

KUMBE HIKI NDICHO KIPAJI KINGINE CHA YAYA TOURE UKITOA MPIRA WA MIGUU, KITAZAME HAPA.


Yaya Toure akiwa na jezi ya timu ya Manchester City.

Yaya Toure, mchezaji mpira wa miguu katika klabu ya Manchester City na timu ya Taifa ya Ivory Coast ana kipaji kingine kikubwa cha mchezo wa Karate.
Mchezo wa Karate alianza akiwa bado kijana mdogo kabisa na huenda pengine ndio angeendelea nao mpaka sasa kama asinge katazwa na baba yake mzee Toure maana ulikua ukimletea majeraha ya mara kwa mara.
Akiwa mdogo aliweza kufanya vizuri sana katika mchezo huo wa Karate mpaka kufikia hatua ya kuchaguliwa katika mashindano makubwa yaliyokua yafanyike Kenya lakini hakuweza kuhuzuria kutokana na kukatazwa na baba yake.
Pamoja na yote bado Yaya Toure ana kipaji cha mpira wa miguu na amekua akifanya vizuri sana ambapo ameweza kutunikiwa tuzo ya uchezaji bora afrika inayo tolewa na BBC kila mwaka.


Yaya Toure akiwa ndani ya jezi ya taifa la ivory coast.

DAH! HII SASA KALI, MAKABURI KUWEKEWA HUDUMA YA INTERNET, SOMA HAPA HABARI NZIMA, HUWEZI AMINI.

DAH! HII SASA KALI, MAKABURI KUWEKEWA HUDUMA YA INTERNET, SOMA HAPA HABARI NZIMA, HUWEZI AMINI.

Chekhov

Makaburi matatu yanayotembelewa sana na watu jijini Moscow yatawekewa huduma ya mtandao ya wi-fi (internet shirikishi).
Wanaotembelea makaburi hayo wataweza kutumia mtandao wa intaneti bila malipo katika makaburi ya Novodevichy, Troyekurovskoye na Vagankovo kuanzia mapema 2016 kwa mujibu wa tovuti ya Moscow City.
Mkuu wa huduma za makaburi mjini Moscow Artem Yekimov anasema lengo ni kusaidia wageni kwenye makaburi hayo kutafuta habari zaidi kuhusu watu mashuhuri waliozikwa humo.
Aidha, kuwafanya wafurahie matembezi yao makaburini.
Kampuni ya mawasiliano ya YS System inasema ilijitolea kuweka huduma ya wi-fi humo baada ya kusikia mipango ya kutenga maeneo ya watu “kutulia kisaikolojia” katika makaburi hayo.
Makaburi ya Novodevichy ni moja ya maeneo yanayotembelewa sana na watalii Moscow.
Miongoni mwa watu waliozikwa humo ni mwandishi Anton Chekhov, kiongozi wa zamani wa muungano wa Usovieti Nikita Khrushchev na rais wa zamani wa Urusi Boris Yeltsin.

Source: BBC SWAHILI